Tanzania emblem

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania


Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA)

Tanzania emblem

Jifunze Kiswahili

Haya ni mafunzo ya utangulizi ambayo yana lengo la kuitambulisha lugha ya Kiswahili na Utamaduni wake kwa washiriki. Kozi hii itamwezesha mjifunzaji kufanya mawasiliano ya msingi na ya kawaida katika Kiswahili

Maeneo muhimu ni kama salamu, kujitambuslisha, na maelezo rahisi ya maisha ya kila siku. Kupitia mbinu mbalimbali za ufundishaji kama vile maigizo dhima, utendaji na michezo ya lugha shirikishi, mjifunzaji atajifunza msamiati wa msingi unaohusiana na hali na matukio ya kila siku na kuchunguza mada zinazolenga kukutambulisha kwa kanuni za kijamii na kiutamaduni za Kitanzania.

Pamoja na shughuli za darasani, mjifunzaji atashiriki katika ziara za kimasomo na shughuli mbalimbali za kijamii ambazo zinalenga kumzamisha kindakindaki katika jamii ili aweze kuzungumza Kiswahili katika mazingira halisi.

MBINU
  1. Mkabala wa kimawasiliano
    • Maigizo
    • Ziara
    • Kazi za vikundi
    • Majadiliano
    • Nyimbo
    • Michezo ya lugha
    • Vitu halisi
    • Video, televisheni na sauti
  2. Uzamishaji
    • Familia mwenyeji
    • Rafiki wa lugha
    • Mazoezi kwa vitendo
    • Kumwalika mgeni
    • Kazimradi
  3. Ujifunzaji wa Hiari
    • Utafiti mdogo
    • Mapitio ya machapisho mbalimbali
    • Kazi za ubunifu

Salamu, kujitambulisha, kuwatambulisha wanafamilia, kuagiza vyakula na vinywaji, kukubaliana bei na kununua dukani au sokoni, kuongelea mambo ya sasa, yaliyopita na yajayo, kusoma saa kwa Kiswahili, kuzungumzia kazi au utaalamu, kuzungumzia matatizo ya kiafya, kutoa na kupokea maelekezo, kuelekeza mahali alipo au kilipo kitu fulani.

Ni watu wasio na ujuzi wa lugha ya Kiswahili, ambao wanaweza kuwa:

  • Wafanyakazi wa maendeleo
  • wamisionari
  • Madaktari
  • Wafanyabishara
  • Wawekezaji
  • Wataalam kutoka nje ya nchi
  • Watafiti
  • Watalii
  • Wanafunzi na yeyote anayehitaji kujifunza lugha ya Kiswahili katika hatua ya kati