Maadili ya Msingi

Ili Baraza liwe  katika mazingira yanayoliwezesha kufikia malengo yake ya kukuza na kusimamia maendeleo ya Kiswahili ndani na nje ya nchi, yafuatayo yatakuwa maadili ya msingi: -

(i) Kukuza ushiriki wa jamii: Kukuza ushiriki wa jamii kuhusu matumizi ya Kiswahili fasaha katika matumizi rasmi;

(ii) Utendaji wa pamoja: Kufanya kazi kwa pamoja kama timu ili kufikia malengo ya Baraza na jamii kwa ujumla;

(iii) Kufanya kazi kwa bidii: Kuongeza juhudi katika kutoa huduma na kuzingatia ubora wa huduma zinazotolewa;

(iv) Uadilifu: Kuwa waadilifu na mfano wa kuigwa katika utendaji kazi;

(v) Uwajibikaji: Kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi;

(vi) Matumizi bora ya rasilimali: Kutumia  kwa uangalifu rasilimali za Baraza kwa manufaa na maendeleo ya lugha ya Kiswahili;

(vii) Uwazi:  Kuzingatia uwazi wakati wa utekelezaji wa majukumu ya Baraza na kuwa tayari kupokea maoni ya jamii; na

(viii) Kukubaliana na mabadiliko: Kuwa tayari wakati wote ili kuendana na mabadiliko.